Wednesday 21 September 2016

WAZIRI NAPE NNAUYE AIPONGEZA KILIMANJARO QUEENS MABINGWA KOMBE LA CECAFA




Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye amewapongeza Wachezaji wa Kilimanjaro Queens kwa niaba ya serikali na kwa niaba ya watanzania kwa kazi nzuri waliyoifanya mpaka kuwa mabingwa wa kwanza wa Kombe la CECAFA kwa mpira wa miguu kwa wanawake Afrika Mashariki na Kati.
Pongezi hizo zimetolewa na Waziri Nnauye alipokua akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam.

“Kama serikali ni vyema kuipongeza timu yetu ya Kilimanjaro Queens kwa kuiwakilisha vizuri Tanzania katika michuano CECAFA na kuibuka mabingwa kwa kuweza kuruka vizingiti vyote vilivyokuwepo katika muchuano hiyo” alisema Mhe. Nnauye
Serikali itaendelea kuweka nguvu ya kutosha na kuungana na timu zetu kuwasaidia kuhakikisha wanafanya vizuri zaidi katika michezo mbalimbali, amesema Mhe. Nnauye.

Mhe. Nnauye amesema kuwa Tanzania inaanza kuona matunda ya uwekezaji wa muda mrefu kwani haikuwa kazi raisi kwa Kilimanjaro Queens kufikia fainali na kuwa mabingwa kwa kupambana na timu ngumu na kuweza kushinda.

Aidha Mhe. Nnauye amewahaidi wachezaji wa Kirimanjaro Queens kuwaalika bungeni katika Bunge lijalo kwa ajili ya kuwapongeza na kuwaandalia mechi ya kirafiki kutambua mchango wao wa kuipeperusha bendera ya Tanzania kati yao na wabunge wanawake.


Timu zilizoshiriki katika michuano ya kombe la chalenji la CECAFA ni pamoja na Tanzania, Burundi, Zanzibar, Kenya, Ethiopia, Rwanda pamoja na mwenyeji Uganda. Mashindano ya Kombe la Chalenji la CECAFA kwa timu za wanawake yamefanyika kwa mara ya kwanza jambo linaloleta tafsiri kuwa michuano hiyo inaweza kuinua soka la wanawake kwa ukanda wa nchi za Afrika Mashariki na Kati.

No comments:

Post a Comment