Wednesday 21 February 2018

MTOTO WA MIAKA SITA AFARIKI WAKATI AKIOMBEWA MAPEPO MKOANI GEITA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita,Mponjoli Mwabulambo akizungumza na waandishi wa habari juu ya tukio la kufariki kwa mtoto wakati alipokuwa akiombewa.
Mtoto wa miaka sita (6) ambaye anajulikana kwa jina la Frank Bariki amefariki wakati alipokuwa akiombewa mlimani alikopelekwa kwaajili ya kutolewa mapepo kwa madai alikuwa na taswira ya Bibi yake,huku mama mzazi  akishikiliwa na jeshi la polisi kwaajili ya upelelezi.

Kamanda wa Polisi mkoani Geita,Mponjoli Mwabulambo alisema Tukio hilo lilitokea february 18,2018 majira ya saa tano asubuhi katika mlima wa Gambiwe  kwenye kijiji cha Bukuru Wilaya ya Nyang’hwale.

Aidha amewataja wanawake hao kuwa  Bi,Neema Petro(25)  ambaye ni mama wa mtoto huyo  na mke mwenzake Raheli Mussa (25)  ambao wameolewa na Bw,Bariki Lunyaru walikuwa kwenye kipindi cha mfungo wakiwa kwenye maombi yao wakati wakimuombea kwaajili ya kumtoa mapepo ndipo walianza kumkamia mtoto huyo wakimshika na kumkaba kwenye mbavu na kwenye shingo hali ambayo ilipelekea mtoto huyo kupoteza maisha.

Kamanda  Mponjoli ameendelea kusema wamechunguza mwili wa mtoto wamebaini kulikuwa na alama   za mikwaruzo kwenye maeneo ya shingoni  na kwenye mashavu .

Ameendelea kufafanua kuwa   hadi sasa bado hawajajua  kiini  cha tukio hilo ambalo limesababisha mtoto huyo kupoteza uhai wakati alipokuwa akifanyiwa maombi ingawa hadi sasa jambo ambalo wamebaini  kuna viashiria vya vitendo vya ushirikina ndani ya familia kutokana na madai ya taswira ya bibi yake  .


Kamanda Mponjoli alisema hadi  sasa wanawashikilia wanawake hao ambao ni wakazi wa kijiji cha Bukulu wilayani Nyang’hwale kutokana na kifo cha mtoto huyo.

No comments:

Post a Comment