Wednesday 21 February 2018

WAZIRI MWAKYEMBE AKUTANA NA WASANII WA SANAA YA UCHONGAJI KUTATUA CHANGAMOTO YA UMILIKI WA ENEO LA MWENGE



Katibu wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza (kulia) akizungumza wakati wa kikao cha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) kujadili mgogoro wa umiliki wa eneo la Mwenge kati ya wachongaji na wafanya biashara wa bidhaa za uchongaji leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Bw. Adrian Nyangamalle



Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akizungumza na wasanii wa sanaa ya uchongaji pamoja na wafanya biashara wa kazi za uchongaji (hawapo pichani) wakati wa kikao cha kujadili mgogoro wa umiliki wa eneo la Mwenge kati ya wachongaji na wafanya biashara wa bidhaa za uchongaji leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Bw. Adrian Nyangamalle



Mwenyekiti mstaafu Chama cha Wasanii Wachongaji Tanzania (CHAWASAWATA) Bw. Focus Senya (kushoto) akitoa ufafanuzi wa mgogoro wa umiliki wa ardhi kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) wakati wa kikao kujadili mgogoro wa umiliki wa eneo la Mwenge kati ya wachongaji na wafanya biashara wa bidhaa za uchongaji leo Jijini Dar es Salaam.

 

Mwenyekiti wa Chama cha Wasanii Wachongaji Tanzania (CHAWASAWATA) Bw. Isihaka Abdul akielezea historia ya umiliki wa ardhi kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) wakati wa kikao kujadili mgogoro wa umiliki wa eneo la Mwenge kati ya wachongaji na wafanya biashara wa bidhaa za uchongaji leo Jijini Dar es Salaam.



Mmoja wa wajumbe wa chama cha Makonde Hand Craft Village Bw. Hamis Mhando (kushoto) akifafanua jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) kujadili mgogoro wa umiliki wa eneo la Mwenge kati ya wachongaji na wafanya biashara wa bidhaa za uchongaji leo Jijini Dar es Salaam.





Baadhi ya wasanii wanaojishughulisha na sanaa ya uchongaji katika eneo la Mwenge wakimsikiliza Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) wakati wa kikao cha kujadili mgogoro wa umiliki wa eneo la Mwenge kati ya wachongaji na wafanya biashara wa bidhaa za uchongaji leo Jijini Dar es Salaam.




Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amesema kuwa tasnia ya sanaa ya uchongaji haiwezi kuendelea kama mgogoro wa umiliki wa eneo la Mwenge utaendelea kuchukua nafasi kubwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku hivyo kushindwa kujiinua kiuchumi na hata kushindwa kuchangia katika pato la taifa.

Waziri Mwakyembe ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam alipokutana na wasanii wachongaji pamoja na wafanyabiasha wa kazi za sanaa ya uchongaji kujadili mgogoro wa umiliki wa eneo la Mwenge ili kuweza kuweka mikakati ya kutatua changamoto hiyo iliyodumu kwa zaidi ya miaka 10.

Waziri Mwakyembe amesema kuwa eneo la Mwenge lenye mgogoro lina uwezo mkubwa chini ya serikali ya awamu ya tano kupata pesa nzuri kutoka kwa wawekezaji na kubadilisha muonekano wake kutokana na eneo hilo kuwa na bidhaa nzuri zinazobuniwa na wasanii wachongaji hivo kuwa kivutio kikubwa kwa watalii kutoka mataifa mbalimbali.

“Tutarudi tena hapa kuja kutoa msimamo wa serikali ni upi ili tuweze kuendelea, hii ni serikali ya awamu ya tano haki lazima itendeke hiki sio kipindi cha wajanja wajanja kuchezea haki za wenzao” amesema Mhe. Mwakyembe

Aidha Mhe. Mwakyembe amewataka wasinii wachongaji  pamoja na wafanyabiashara wa kazi za sanaa ya uchongaji kuwa na umiliki wa pamoja na kutambuana kama watoto wa baba mmoja na mama mmoja ili kuweza kuiendeleza tasnia hiyo ya uchongaji kwa maslahi yao na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Katibu Baraza la Sanaa la Taifa Bw. Godfrey Mngereza amesema kuwa lengo la kujadili sintofahamu ya eneo la Mwenge ni  pamoja na kurekebisha sintofahamu hiyo ili wasanii wachongaji pamoja na wafanyabiasha waweze kwenda kwa pamoja katika kujenga nchi hii kwani sanaa ni kazi, sanaa ni uchumi lakini pia sanaa inazalisha ajira.

Naye Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Bw. Adrian Nyangamalle amesema kuwa nia kubwa ya shirikisho hilo ni kuifanya tasnia ya sanaa za ufundi kufika mahala ambapo italeta mchango unaokusudiwa kwa taifa na kubadilisha maisha ya wasanii na wadau wote wa tasnia hiyo na hili hayo yafikiwe ni lazima kuwe na amani ili kila mtu awe na uhuru wa kufanya kazi zake kwa nafasi.  


Aidha Bw. Nyangamalle amesema kuwa Shirikisho la Sanaa za Ufundi limeweza kupokea changamoto ya umiliki wa ardhi hiyo na kuwasilisha kwa wadau na serikali kwa ajili ya kusaidia kutatua changamoto hiyo.



No comments:

Post a Comment