Tuesday 6 February 2018

MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WATAKIWA KUBUNI MBINU ZA MAENDELEO

rc
Mkuu wa mkoa wa Geita ,Mhandisi Robert Luhumbi akizungumza na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Geita juu ya kuendelea kuwatumia   mafundi wa ngazi za mitaa (Local fundi) kwenye miradi ya jamii. 

DSC_1761
Mwenyekiti wa halmashauri  ya wilaya ya Geita ,Elisha Lupuga akizungumza na madiwani wakati wa kikao cha kawaida cha robo ya pili cha baraza hilo. 

DSC_1766
Madiwani wakiwa kwenye  kikao cha kawaida cha robo ya pili cha baraza. 

DSC_1771


Na Maduka Joel, Geita
Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Geita wametakiwa kubuni mbinu zitakazoleta Maendeleo kwenye Kata zao pamoja na kushughulikia utatuzi wa kero za wananchi kwenye maeneo yao.

Akizungumza wakati wa kikao cha kawaida cha robo ya pili cha baraza la madiwani  Mwenyekiti wa halmashauri  hiyo Bw Elisha Lupuga amewataka Madiwani hao kuwatumikia wananchi kikamilifu na kuachana na mambo yanayoweza kuzorotesha maendeleo.

“Kipindi hiki ni cha kufanya kazi na kuwatumikia wananchi Utakiwi kuwa diwani wa kulalamika kwani ukuchaguliwa na wananchi hili uwe kiongozi wa ambaye unakuwa na malalamiko bila ya kutafuta njia ambazo zinaweza kusaidia kutatua changamoto za wananchi ambao unawaongoza natambua Rais wetu kwasasa anasisitiza tufanye kazi za kuwatumikia wananchi wetu” Alisisitiza Lupuga.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi aliwataka madiwani na wataalamu wa Halmashauri ya wilaya ya Geita kufanya kazi kwa ushirikiano kuhakikisha wilaya hiyo inapiga hatua na kuchochea maendeleo ya wananchi.

Pia amesisitiza suala la kutumia mafundi wa ngazi za mitaa katika kukamilisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya shule na afya ili kupunguza gharama za wakandarasi ambao hutoza fedha nyingi.

Mhandisi Luhumbi pia amewakumbusha madiwani kuhoji miradi yote kwenye kata zao na Halmashauri kwa ujumla ambayo inafadhiliwa na mgodi wa dhahabu wa Geita, GGM kwa madai kuwa baadhi ya miradi imekua na gharama kubwa kuliko uhalisia wake.

No comments:

Post a Comment