Monday 12 February 2018

KUKAMILIKA UWANJA WA NDEGE CHATO KUTAFUNGUA FURSA ZA UTALII GEITA

Mwenyekiti  wa    wa Bodi ya Shirika la kuhifadhi Wanyamapori Tanzania (TANAPA),  Jenerali Mstaafu,George Waitara  akizungumza na Mhandisi  wa  ujenzi  wa  uwanja  huo,Makuye Muhinga juu ya mikakati ambayo inaendelea ya ujenzi wa uwanja wa ndege Wilayani Chato mkoani Geita,wakati walipoutembelea.

Barabara  ya  kutua ndege  (run away) yenye  urefu wa  Mita  300  ambayo kwa sasa  hipo  kwenye hatua nzuri za mwisho kukamilika.

Baadhi ya watendaji na wajumbe wa Bodi ya TANAPA wakikagua ujenzi wa mradi wa uwanja wa Ndege Wilayani Chato Mkoani Geita.

Mwenyekiti  wa  bodi  ya   hifadhi za Taifa  nchini (TANAPA),  Jenerali Mstaafu,George Waitara  akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Chato (Katikati) Shaaban Ntarambe pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi ,Robert Gabriel Luhumbi wakati walipofika na kujionea ujenzi wa uwanja wa ndege ambao unajengwa Wilaya ya Chato unavyokwenda kwa kasi.

Mhandisi  wa  ujenzi  wa  uwanja  huo,Makuye Muhinga akizungumza na Mwenyekiti  wa  bodi  ya   hifadhi za Taifa  nchini (TANAPA),  Jenerali Mstaafu,George Waitara   pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Gabriel,Juu ya hatua ambazo wamezifikia hadi sasa za ujenzi wa uwanja wa  Ndege.

 


Na Joel Maduka, Chato

Kukamilika kwa ujenzi  wa uwanja  mkubwa wa ndege wilayani Chato mkoani Geita unatarajia kuwavutia watalii wengi kutembelea  kivutio cha hifadhi ya Taifa cha Rubondo Kilichopo mkoani humo  .

Ujenzi wa uwanja huo  umeanza rasmi mwezi wa Septemba mwaka jana na unatarajia kukamilika Juni mwaka huu.

Hayo  yamesemwa    na  Mwenyekiti  wa  bodi  ya wadhamini (TANAPA),  Jenerali Mstaafu George Waitara  wakati  alipotembelea uwanja huo pamoja na wajumbe wa  bodi  hiyo  na baadhi  ya watendaji  kwa nia  ya   kujionea maendeleo  ya  ujenzi  huo  ambao  umeelezwa  kukamilika kwa  asilimia  65.

“ Kiukweli niseme kazi  kubwa sana ambayo imefanyika  ya ujenzi wa uwanja huu utakuwa na faida kubwa sana kwaajili ya mambo ya utalii na mambo mengine kama ya biashara na suala jingine kubwa ni kuibua vivutio vingine tupate watalii wengi zaidi  , tunatarajia  utakapokamilika  utaleta  manufaa sana  katika  sekta  mbali mbali  zikiwemo  za  utalii  na  biashara  mkoani  Geita  na  mikoa  ya  jirani,” Alisema Waitara.

Kwa  upande  wake,  Mhandisi  wa  ujenzi  wa  uwanja  huo,Makuye Muhinga,Alisema uwanja  huo wenye  barabara  ya  kutua ndege  (run a way ) yenye  urefu wa  Mita  300  upo  kwenye hatua nzuri na kwamba wanatarajia kukamilisha   mwaka  huu ujenzi wa uwanja.

Aidha   Mkuu  wa  Mkoa  wa  huo   ,  Mhandisi  Robert  Gabriel Luhumbi   ambaye alikuwa ni miongoni mwa watu ambao wametembelea uwanja huo alisema kukamilika kwa uwanja huo kutafungua uwigo mpana wa kiuchumi kutokana na kwamba mkoa utaweza kutembelewa na wageni kutoka mataifa ya nje na jirani.

“Wito wangu kwa wananchi ni kuhakikisha wanachangamkia     fursa  mbalimbali  za  maendeleo  hasa  uanzishwaji  wa  viwanda  vidogo vya  kuchakata  mazao  yalimwayo  mkoani  humu, na tunaamini  uwanja  huu utarahisisha  usafirishaji  wa  bishara  ambazo watakuwa wanazifanya badala ya kupitia Mwanza sasa hivi wataweza kupitia kwenye mkoa wao”Alisema Luhumbi.

Jumla ya hifadhi zilizopo nchini ni 16 ambazo zinatambulika kimataifa ikiwemo na hifadhi ya Rubondo ambayo hipo Mkoani Geita.

No comments:

Post a Comment