Monday 11 July 2016

SERIKALI YA INDIA NA TANZANIA KUSHIRIKIANA KUTEKELEZA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO



Waziri Mkuu wa India Narendra Modi akikagua gwaride la heshima mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Leo Jijini Dar es Salaam.



Waziri Mkuu wa India Narendra Modi na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli wakiimba nyimbo za mataifa ya India na Tanzania, leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.



Waziri Mkuu wa India Narendra Modi na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli wakiwasalimia na baadhi ya Watanzania waliojitokeza wakati Bw. Narendra alipowasili katika viwanja vya leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.




Waziri Mkuu wa India Narendra Modi na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli wakipiga ngoma wakati Waziri Mkuu Narendra alipowasili katika viwanja vya Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.


Waziri Mkuu wa India Narendra Modi na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali ya Tanzania na India wakiwa katika mazungumzo maalum Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.


Waziri Mkuu wa India Narendra Modi akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari ambapo ameahidi kusaidia katika utekelezaji wa Miradi ya Maji katika Miji ya Dar es Salaam na Pwani, pia kusaidia katika kuendeleza sekta za Habari na Mawasiliano, Viwanda Vidogo vidogo na Vyakati, Kilimo, Afya na masuala ya Usalama nchini, Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akiongea na waandishi wa habari wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa India Narendra Modi ambapo ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa nchi hiyo katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo na kumshukuru Bw. Narendra kwa utayari wa kusaidia utekelezaji wa Miradi mbalimbali nchini.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Dkt. Aziz Mlima na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje wa India Bw. Amar Sinna wakionesha ramani inayoonesha maeneo ya Nchi yaliyozungukwa na bahari wakati wa Ziara ya Waziri Mkuu wa India Narendra Modi leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi wakigongesha Glasi kutakiana Kheri.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akimpa Mkono Waziri Mkuu wa India Narendra Modi mara baada ya kumalizika kwa mkutano na vyombo vya habari Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akimshukuru Waziri Mkuu wa India Narendra Modi kwa kufanya Ziara nchini Tanzania na kuahidi utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo nchini wakati wa Chakula cha Mchana leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Waziri Mkuu wa India Narendra Modi akiongea na baadhi ya wageni walioalikwa kwenye Chakula cha Mchana Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi alipowasili Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akifanya Mazungumzo na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi alipowasili Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.


Waziri Mkuu wa India Narendra Modi akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa chakula cha Mchana Ikulu leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli.



Waziri Mkuu wa India Narendra Modi akisalimiana na akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Warioba wakati wa chakula cha Mchana Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.


No comments:

Post a Comment