Thursday 4 January 2018

WAZIRI MWIJAGE ASISITIZA UANZISHWAJI WA VIWANDA VIDOGO MKOANI GEITA

DSC_0904
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe..Charles Mwijage akizungumza na wadau wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji  wa Ppamoja na wananchi Wilayani Chato  Mkoani Geita wakati alipokuwa kwenye ziara ya kutazamana na kukabidhi maeneo ambayo yatajenga majengo ya kufindishia wajasiliamali.


DSC_0800
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akisoma taarifa ya Mkoani huku akisisitiza namna ambavyo Mkoa huo umejipanga kuendelea kupanua zaidi sekta ya viwanda kwenye halmashauri zilizopo ndani ya Mkoani hu.

DSC_0805
Baadhi ya wajumbe na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoani na Wilaya ya Geita wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo,Mhandisi Robert Luhumbi wakati alipokuwa akisoma taarifa ya Mkoa.

DSC_0828
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe..Charles Mwijage akisisitiza ujenzi wa haraka zaidi  wakati alipotembelea eneo la magogo lililopo kwenye halmashauri ya Mji wa Geita.

DSC_0917
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe..Charles Mwijage akizungumza na wananchi Wilayani Chato  Mkoani Geita kwenye eneo ambalo linatarajia kujengwa mradi wa majengo ya kufundishia wajasiliamali.



Na, Joel Maduka, Geita.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage   Amesema lengo la  Serikali ni kuhamasisha ujenzi wa Uchumi wa Viwanda Jumuishi ambao unawahusisha watu wengi kupitia viwanda vidogo na vya kati,vitakavyotumia malighafi zitakozozalishwa hapa nchini vilivyopo katika maeneo mbalimbali nchini,  ukiwepo mkoa wa Geita ambao umeonekana kufanya vizuri katika eneo hilo.

Waziri Mwijage ameyasema hayo alipozungumza na wadau wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji wa Mkoa wa Geita  wakati wa ziara yake Mkoani humo, ambapo amesisitiza  juu ya Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda ulio imara, shindani na endelevu, utakayozingatia mambo muhimu matatu ambayo ni soko, malighafi na teknolojia.

Sanjali na Hayo Waziri Mwijage amemtaka  mkuu wa mkoa kuhakikisha anasimamia vyema ujenzi wa ofisi za  SIDO pamoja ujenzi wa majengo ya kufundishia wajasiriamali ambayo yanatarajia kujengwa Wilayani Chato ili kufikia mwezi wa nne ujenzi huo uwe umekamilika .

Pia ameongezea kuwa ujenzi wa ofisi ambazo zitajengwa kwenye eneo la magogo litakuwa na eneo la  kuwafundishia wajasiriamali mbinu mbali mbali za kuanzisha viwanda vidogo pamoja na namna ya kusindika bidhaa ambazo wanatakiwa  kuziingiza sokoni.

Akiwasilisha taarifa ya Mkoa ,Mkuu wa Mkao wa Geita Mhandisi Robert Luhumbi,  amesema ili kuandaa mazingira mazuri yatakayowawezesha wawekezaji kuvutiwa na kuwekeza mkoani humo  Mkoa umetenga maeneo 384 yaliyopo katika Halmashauri sita yenye ukubwa wa jumla ya ekari 1,012 kwa ajili ya viwanda na ramani za mipango miji zimeandaliwa .

Luhumbi ametaja mikakati ya mkoa huo kwenye sekta ya viwanda kuwa ni Kuanzisha kiwanda cha kuchakata muhogo na kufungasha ambapo maghala mawili  ya kuhifadhi muhogo na sokomoja  yamejengwa na kukamilika kupitia Programu ya Uboreshaji wa miundombinu ya masoko uongezaji thamani na huduma za kifedha vijijini pia Kuanzisha kiwanda cha kusindika nyama katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe ambapo andiko limeandaliwa na kuwasilishwa katika Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa ajili ya kupata mwekezaji.

Ameongezea kuwa Mkoa unaendelea kufanya mazungumzo na wawekezaji walioonesha nia ya kuwekeza katika kiwanda cha sukari. Aidha, tarehe 02 Januari, 2018 Mkoa umekutana na uongozi wa Bodi ya Sukari Tanzania kwa lengo la kuanzisha kiwanda cha sukari katika Wilaya ya Geita.


Ofisi hizo zinazotarajia kujengwa kwenye eneo la Magogo kwenye halmashauri ya  mji wa Geita na Wilaya ya Chato zinatarajia kuwa  na maabara ndogo kwa ajili ya uzalishaji,Chumba cha baridi kwa ajili ya kuhifadhi bidhaa kama maziwa na kadhalika na kutakua na mabanda ya watakayotumia wajasiriamli kwa muda.

No comments:

Post a Comment