Thursday 25 January 2018

MILA POTOFU NA UMBALI IMEELEZWA NI SABABU WAJAWAZITO KUJIFUNGULIA NYUMBANI

DSC_0823
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha afya cha Uyovu Wilayani Bukombe,Dk Steven  Kazuzu akisoma taarifa mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Geita,wakati alipofika kushiriki ujenzi wa jengo la upasuaji.

DSC_0699
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akisaini kwenye kitabu cha wageni ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Bukombe wakati alipowasili 

DSC_0731
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe,Josephat Maganga akisisitiza wananchi kuendelea kushiriki kwenye shughuli za maendeleo ambazo zinafanywa na serikali ya awamu ya Tano.

DSC_0769
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akiweka sawa mawe kwenye msingi wa shule ya Sekondari ya Ushirombo wakati alipofika kushiriki na wananchi shughuli za maendeleo.

DSC_0782
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akizungumza na wananchi pamoja na wakina mama ambao wananufaika na mfuko wa TASAF wilaya ya Bukombe.


DSC_0813
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe,Safari Mayala akizungumza na wananchi wa uyovu juu ya maendeleo.

DSC_0835
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akisisitiza ushiriki wa wananchi kwenye sekta ya maendeleo kwenye maeneo ambayo wanaishi.

Na Joel Maduka, Bukombe. 

Mila potofu na umbali wa vituo vya afya zimetajwa kuwa kati ya sababu za baadhi ya wajawazito kujifungulia nyumbani wanapopatwa na uchungu katika Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita.

 Mganga Mfawidhi wa Kituo cha afya cha Uyovu Wilayani Bukombe Dr Steven Kazuzu alisema  uelewa wa wananchi kuhusu kujifungulia kwenye vituo vya afya ni mdogo na kwamba wengine wamekuwa na imani potofu kwamba Mwanamke anapojifungulia nyumbani kuna baadhi ya viungo hubaki navyo tofauti na akijifungulia hospitalini.

“Tatizo kubwa ambalo linasababisha wakina mama kujifungulia nyumbani ni kuwa na elimu ndogo na kutokujua umuhimu wa kujifungulia kwenye vituo vya afya na wengine wamekuwa na dhana ya kuwa hospitali hawezi kupata vitu ambavyo wanavitumia kwenye mambo yao ya kishirikina hivyo hujikuta wanawalazimisha wakina mama kujifungulia Nyumbani” Alisema Dr Kazuzu.

Bi Mery Musa ambaye ni mkazi wa Uyovu alisema  tatizo kubwa ni ukosefu wa elimu na vifaa kwenye baadhi ya zahanati hali inayosababisha wengi wao kutoona umuhimu wa kujifungulia kwenye vituo vya huduma za afya.

Akiwa kwenye ziara wilayani Bukombe, Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel alisema lengo la serikali ni kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa kwa kuwa na majengo ya kutosha na vifaa tiba pia.

No comments:

Post a Comment