Thursday 4 January 2018

SERIKALI YAOMBWA KUTEKELEZA MIRADI YA MAJI KWA WAKATI WILAYANI CHATO, GEITA

3526482_orig
Moja kati ya mwananchi akichota maji kwenye kisima ambacho ni cha kienyeji.

DSC_0378
Mbunge wa Jimbo la Chato,Dkt,Medard Kalemani akizungumza na wananchi wa Kata ya Ilemela Juu ya juhudi ambazo zinafanywa na serikali ya awamu ya tano katika kutatua kero ya maji.

Na, Joel Maduka, Geita

Wakazi wa Wilaya ya Chato Mkoani Geita,wameiomba serikali kutekeleza kwa haraka miradi ya maji iliyoahidiwa kwa muda mrefu kutokana na watu wengi kupata shida ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji

Baadhi ya wananchi hao Bi Anastazia Mashauri ambaye ni mkazi wa Kata ya Ilemela na Bahati Mashauri ambaye ni mkazi wa Kata ya Muungano wameelezea kuwa pamoja na jitihada ambazo serikali imeendelea kuzifanya kuwapatia maji lakini hali bado mbaya kwani wengi wao hawapati maji safi na salama.

"Hali ya upatikanaji maji kijijini kwetu ni mbaya sana kwani tunakisima kimoja tu hali ambayo imekuwa ikisababisha wengi wetu kuelekea ziwani kutafuta maji na maji ambayo tunachota ya ziwani yanakuwa sio masafi ila inaturadhimu kuchota tu kutokana na shida ya maji tunyopata hapa kijijini kwetu tunaomba serikali itusaidia kiukweli tunapata shida sana" Alisema Bi Annastazia Mashauri.

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Bw Bathoromeo Manunga amesema wanatarajia kutekeleza Miradi mikubwa miwili ya maji ambayo itawanufaisha Wakazi elfu 62 ambapo kwa sasa ni asilimia 42 ya wakazi wanaopata maji na salama.

Ameongeza kuwa mradi mmoja kati ya hiyo unategemea kuchukua maji kutoka ziwa Victoria ambao utasambaza maji katika maeneo mbalimbali Wilayani Chato.

Mbunge wa Jimbo hilo Dr Medard Kalemani amewaambia Wananchi wa Ilemela, Nyamboge na Kanyama kuwa awali walileta mradi wa visima vya kina kirefu lakini bahati mbaya Mkandarasi alipokuja ilikua kipindi cha ukame na maji hayakutoka na January 7 2018 Mkandarasi anakuja kupima tena.

No comments:

Post a Comment