Wednesday 10 January 2018

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AKERWA NA KUTOKAMILIKA KWA MIRADI YA MAJI MKOANI GEITA

DSC_0726
Waziri wa maji na umwagiliaji Bw Isack Kamwelwe  akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Luhumbi wakati alipowasili kwenye  ofisi za Mkoa huo.

DSC_0739
Waziri wa maji na umwagiliaji Bw Isack Kamwelwe ,akisalimiana na mbunge wa Jimbo la Busanda Lolesia Bukwimba wakati alipowasili kwenye ofisi za Mkoa wa Geita. 

DSC_0831
Mkuu wa Mkoa wa Geita ,Mhandisi Robert Luhumbi akielezea hali ilivyo ya upatikanaji wa maji wakati wa kikao na wadau wa sekta ya maji Mkoani humo.

DSC_0843
Waziri wa maji na umwagiliaji Bw Isack Kamwelwe,akizungumza na wadau wa sekta ya maji kwenye ukumbi wa mikutano wa mkoa wa Geita. 

DSC_0851
Baadhi ya wadau wa sekta ya maendeleo na wenyeviti wa halmashauri za wilaya  pamoja na wakurugenzi wakiwa kwenye mkutano wa Waziri wa maji na umwagiliaji Bw Isack Kamwelwe ambao ulikuwa unajadili mstakabali wa  upatikanaji wa maji kwenye mkoa wa Geita. 

DSC_0870
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM)Mkoa wa Geita,alhaji Said Karidushi  akiwasisitiza watumishi kusimamia kwa makini zaidi miradi ya maji iliyopo kwenye Mkoa huo.

DSC_0881
Waziri wa maji na umwagiliaji Bw Isack Kamwelwe akiwa kwenye mradi wa maji uliopo kwenye kata ya Kalangalala. 

DSC_0889

Waziri wa maji na umwagiliaji Bw Isack Kamwelwe ameeleza kusikitishwa na  kitendo cha kutokamilika kwa miradi ya maji ya Inchukimya Bulamabupina, Nchankolongo na Nyamtukuza licha ya serikali kutenga fedha nyingi kugharamia  miradi hiyo.
Akizungumza na wadau wa maji, Mkoani Geita katika ukumbi wa Ofisi ya Mkoa huo Bw Kamwelwe amesema amesikitishwa na mradi wa wilaya ya Nyang'hwale ambao umegaramiwa Sh Bilioni 15 ambao hadi sasa umeshindwa kukamilika licha ya mikataba zaidi ya kumi na moja kusainiwa.

Amesema lengo la serikali ni kuona kufikia mwaka 2020, Watanzania hususani wa vijijini wamepata Asilimia 85 ya maji safi na salama.

“Mimi nimepewa dhamana ya kuhakikisha watanzania wanapata maji safi na salama na ifikapo mwaka 2020 vijijini wapate asilimia themanini na tano kwasababu serikali yetu inatenga bajeti ya utekelezaji wa miradi hii” alisema Kamwelwe.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Luhumbi amemwambia Waziri kuwa mkoa huo una tatizo la upatikanaji wa maji kwenye maeneo mengi licha ya kuzungukwa na chanzo kikubwa cha maji ya ziwa viktoria.

Mbunge wa Busanda Lolesia Bukwimba akizungumza kwa niaba ya wabunge wa Mkoa huo, alisema anaamini ziara ya Waziri wa maji na umwagiliaji itasaidia kutatua kero ya maji inayowasumbua wananchi kwa muda mrefu kwenye mkoa huo .


Waziri wa maji na umwagiliaji Bw Isack Kamwelwe yuko Mkoani Geita kwa ziara ya siku 4 yenge lengo la kukagua miradi ya maji


No comments:

Post a Comment