Sunday 27 May 2018

VIJANA MKOANI GEITA WASHAURIWA KUFANYA KAZI KWA BIDII


Baadhi ya Vijana wa mtaa wa Bugayambelele Kata ya Lutede mkoani Geita wameshauriwa kuachana na michezo ya Pool table na kamali na badala yake wajichanganye katika shughuli ndogo ndogo zitakazo waingizia kipato cha halali.

Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi Ccm tawi la Bugayambelele Bw Aniset Ngaiza wakati akizungumza na Mwandishi wtu mtaani humo ambapo amesema vijana wengi katika eneo hilo hawataki kufanya kazi kwa bidii na badala yake kushinda kwenye vijiwe vya pool table pamoja na kamali.

Bw Ngaiza amesema chama cha mapinduzi Ccm katika tawi hilo kimejipanga kuhakikisha kina washawishi baadhi ya vijana hao kuendelea kuepuka michezo hiyo kwa kuwa nguvu ya kijana ni muhimu katika ujenzi wa taifa.

Kwa upande wake katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi Ccm katika tawi hilo Bw Ally Bigambo amewashauri wazazi na walezi kupunguza majukumu na kuwa karibu na watoto wao muda mwingi ili kuendelea kuepuka kizazi kisicho penda kufanya kazi.


No comments:

Post a Comment