Friday 25 May 2018

TAMKO LA KOREA KASKAZINI BAADA YA TRUMP KUFUTA MKUTANO NA RAIS KIM


Leo May 25, 2018 Serikali ya Korea Kaskazini imesema kwamba iko tayari kufanya mazungumzo na Washington wakati wowote kutatua matatizo kati yao, baada ya Marekani kuufutilia mbali mkutano wa kihistoria kati ya viongozi hao wawili.
Korea Kaskazini ilionyesha majuto juu ya uamuzi wa Rais wa Marekani Donald Trump kusitisha mkutano huo ambao ulikuwa umepangwa kufanyika June 12, 2018 nchini Singapore, Waziri wa Kwanza wa Makamu wa Nje, Kim Kye Gwan alisema.

Siku ya Alhamisi Rais Trump alimtumia Kim Jong Un barua ya kuufutilia mbali mkutano huo.

No comments:

Post a Comment