Friday 14 July 2017

WANANCHI MKOANI GEITA WALILIA MAFUTA







Kufuatia agizo la Waziri wa Fedha na Mipango,Dk Philip Mpango la kuzitaka mamlaka za mapato Nchini (TRA)kufanya ukaguzi nchi nzima ili kubaini  wamiliki wa vituo vya mafuta wanaokiuka maagizo ya serikali yaliyowataka wafunge mashine maalum za kielektroniki za kutolea risiti(EFD)tangu mwaka jana.
Baadhi ya watumiaji wa Huduma ya Mafuta  Wilaya na Mkoa wa Geita,Bi  Julian Kimaro na Halfan Rajabu ,wamesema kukosekana kwa Huduma  hiyo wameathirika kwa kiasi kikubwa kwani  tangu siku ya jana majira ya jioni na alfajiri  ya saa kumi wamekuwa kwenye foleni wakisubiri kupata mafuta na kwamba ni  Kituo kimoja tu ndicho ambacho kinatoa huduma  hiyo.  

Baadhi ya  Mameneja wa vituo vya mafuta  Moil na Tropical ,James Zabron na Ismail Adam,wamesema kuwa wameenda Kwenye mamlaka ya mapato kununua mashine hizo lakini hawajazipata kwa madai kuwa hata TRA pia hawana mashine hizo na tatizo lipo kwa mafundi wa kufunga kwenye injini za mafuta.

Mwenyekiti wa chama cha wamiliki na waendeshaji wa vituo vya mafuta(TAPSOA) mkoani Geita, Hamis  Tabasamu amesema kuwa  tatizo ni bei ya mashine hali ambayo imewafanya wafanyabiashara walio wengi kushindwa kununua mashine hizo.

Meneja wa TRA Mkoani Geita,Samuel Nkonya amesema kuwa zoezi ambalo linaendelea  ni la kufanya ukaguzi kwenye vituo vyote lengo likiwa ni wamiliki kuwa na mashine za kutoa risiti ambazo zinafungwa kwenye Mtambo wa utoaji wa mafuta na kwamba  jumla ya vituo 18 hadi sasa vimefungwa na kituo ambacho kinafanya kazi ni kimoja tu.


Zoezi la kufunga vituo vya mafuta ambavyo havina mashine za EFD ni la nchi nzima 

No comments:

Post a Comment