Tuesday 18 July 2017

SERIKALI WILAYANI GEITA KUFIKISHA NISHATI YA UMEME KATA YA KASEME



Baadhi ya wananchi wakiwa kwenye Kisima cha maji ambacho kimejengwa na mgodi wa Nyamutondo kwenye Kata ya Kaseme Wilayani Geita.


Mkuu wa Wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi akikagua moja kati ya visima ambavyo aliagiza vijengwe kwenye Kijiji Nyamutondo na mwekezaji ambaye ni mchimbaji mdogo.


Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akimuuliza moja kati ya wananchi wa Kijiji hicho Bi, Koku Gerevasi,kama amelizishwa na visima ambavyo vimetengenezwa na Mgodi wa  Nyamutondo.


  Mkurugenzi wa Mgodi wa dhahabu wa Nyamutondo Bw.Martin Benda Kajoro,akikabidhi visima hivyo Kwa Mkuu wa Wilaya ya Geita na Kuomba radhi kutokana na kushindwa kutekeleza agizo lake la mara ya kwanza. 


Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akizungumza na wananchi na kutoa maelekezo ya kutunza visima ambavyo vimejengwa kwa gharama kubwa.


Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akikata utepe ishara ya kuzindua visima hivyo.


Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi,akimtwika ndoo ya maji baada ya kuzindua visima hivyo


Serikali wilaya ya Geita  kufikisha nishati ya Umeme katika Kitongoji cha Nyamutondo kijiji na kata ya  Kaseme kabla ya Mwezi Oktoba mwaka huu ili kuwezesha Pampu za visima vya maji kutumia Umeme na kusambaza maji kuwafikia wananchi kwa urahisi zaidi.

Hatua  hiyo ya Serikali imekuja ni baada ya Kukamilika kwa Ujenzi wa Visima viwili kati ya vinne ambavyo vimechimbwa na wawekezaji wa mgodi wa dhahahu wa Nyamutondo uliopo Kijiji hicho ambavyo vimejengwa kwa gharama ya shilingi Milioni hamsini  na nne (54).

Akizindua visima hivyo na Kukabidhi kwa serikali ya Kijiji  Mwl.Herman Kapufi ,amesema uwezo wa kusukuma maji kwa sasa katika visima hivyo ni mdogo kutokana na pampu ambazo wananchi wanazitumia kwa mikono na kwamba kupatikana kwa nishati ya umeme kutarahisisha na kuboresha huduma ya maji

“Kazi yangu ni kuhakikisha umeme unaletwa hapa ili kurahisisha swala la maji na kufikia mwezi wa Kumi umeme utakuwa umefika kwenye kijiji hiki”Alisema Kapufi.

Naye Mkurugenzi wa Mgodi wa dhahabu wa Nyamutondo Bw.Martin Benda Kajoro amesema kukamilika na kuzinduliwa kwa visima hivyo kutaondoa changamoto ya maji kwa wananchi iliyopelekea kufungwa kwa shughuli za uchimbaji wa dhahabu kushinikiza wawekezaji kuchimba visima.    

“Kweli kulikuwa na shida kubwa sana ya maji lakini kutokana na hali hiyo Mkuu wa wilaya alituagiza kujenga visima virefu vya maji na sisi tulitilia maanani agizo lake na ndio maana leo (jana) tumemaliza na tumekabidhi kwake hivyo tunamwomba tu afikishe kwa afisa madini aweze kutufungulia mgodi wetu maana kwa sasa hatufanyi shughuli zozote”Alisema Kajoro

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho ambao wamezungumza na mtandao wa maduka online ,Semeni John   na Koku Gerevasi wamesema   walikuwa wakikabiliana na changamoto ya kukaa kwenye foleni kwa muda mrefu na wakati mwingine kujikuta wakikabiliana na vurugu.


No comments:

Post a Comment