Wednesday 20 September 2017

MBUNGE ZITTO KABWE AMEKAMATWA NA POLISI JIONI YA LEO



Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe amekamatwa na jeshi la polisi usiku huu katika uwanja wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam akitokea Kigoma.
Afisa Habari wa Chama Cha ACT Wazalendo, Abdallah Khamis amethibitisha kukamatwa kwa kiongozi huyo wa chama chake na kusema kuwa kwa sasa wanasheria wa chama hicho wanafuatilia kujua sababu ya kiongozi wa chama chao kukamatwa na jeshi la polisi.

"Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, ndugu Zitto Kabwe amekamatwa na Polisi muda huu uwanja wa ndege wa JNIA, Dar es salaam wakati akitoka Kigoma. Kwa sasa wanasheria wa chama wanafuatilia kujua sababu za kukamatwa kwake" alisema Abdallah Khamis


Asubuhi ya leo kulikuwa na taarifa kuwa Katibu wa Bunge Dkt. Thomas kashililah alitoa amri kwa jeshi la polisi kumkamata Mbunge huyo wa Kigoma Mjini na kutakiwa kumfikisha mjini Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa kutokana na kauli ambazo amewahi kuzitoa juu ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu Job Ndugai pamoja na Bunge lenyewe.

No comments:

Post a Comment