Tuesday, 10 January 2017

MTI WAZUA KIZAZAA MKOANI GEITA



Katika hali isiyo ya kawaida wananchi wa mtaa wa samina kata ya mtakuja wilaya na Mkoa wa Geita  wamejikuta wakiingiwa na taaruki ni baada ya mti  mbwa ulionguka kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita kukuta  umesimama  wenyewe.

Friday, 6 January 2017

DC GEITA AKUBALIKA KWA WANANCHI KUTOKANA NA UTENDAJI WAKE WA KAZI


Baadhi ya wananchi wa kata ya Katoro wakimsikiliza kwa makini mkuu wa wilaya ya Geita ,Mwl Herman Kapufi wakati alipokuwa akizungumzia swala la ushiriki wa wananchi katika uchangiaji wa maendeleo katika kata hiyo




Baadhi ya wananchi wakifatilia kwa makini kilichokuwa kikizungumzwa katika mkutano 

Wednesday, 4 January 2017

MAAMUZI YA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA KUHUSU MAUAJI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI



Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba alifika katika kijiji cha Tindiga kilichopo wilaya ya Mikumi zilipotokea vurugu zilizopelekea mkulima mmoja kuchomwa mkuki mdomoni na kutokea shingoni na kusikiliza kero zinazowasumbua wananchi wa Kilosa kabla ya kutoa maamuzi. 

MAUAJI KWA WALINZI YAENDELEA KUWA TISHIO MKOANI GEITA



Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl. Herman C. Kapufi

 Mauaji ya walinzi mkoani Geita yamendelea kuwa tishio kwa usalama wao baada ya mlinzi mwingine aliyekuwa akilinda maduka yapatayo 15, kuuawa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali kichwani. 

Monday, 2 January 2017

MOTO WATEKETEZA MADUKA 14 ARUSHA



Maduka 14 katika eneo la Mianzini jijini Arusha yameteketea kwa moto jana asubuhi na kusababisha hasara mbalimbali huku jeshi la polisi likiimarisha ulinzi na kusimamia shughuli za uokoaji wa mali zilizosalimika. 

MTOTO AMUUA BABA YAKE NA KUTAKA KUMFUKIA



Jeshi  la Polisi mkoani Ruvuma linamshikilia Patrick Malindisa (29) mkazi wa Mtaa wa Namanyigu Manispaa ya Songea kwa tuhuma za kumuua baba yake mzazi Athanasi Malindisa (70) kwa kumpiga na kitu chenye ncha kali kichwani na kidevuni na kisha kutaka kuufukia kwenye shimo alilochimba ndani ya nyumba yao.

MKULIMA AFUNGA SAFARI KUTOKA URAMBO MPAKA BUKOBA KUMUONA RAIS MAGUFULI


Mkulima wa tumbaku aliyesafiri kutoka Wilaya ya Urambo mkoani Tabora, Moshi Rubibi akitafuta upenyo wa kumfikishia Rais John Magufuli kilio cha wakulima, alifanikiwa kufanya hivyo mjini Bukoba  wa kutumia staili iliyomvuta Rais kumsikiliza.