Tuesday 18 October 2016

WANAFUNZI SHULE YA SEKONDARI GEITA BADO NI CHANGAMOTO KATIKA UTOVU WA NIDHAMU


Shule ya sekondari Geita iliyopo Wilayani na Mkoani geita ni moja kati ya shule ambazo zimeendelaea kuwa na changamoto nyingi moja wapo ni wanafunzi  kugoma, kuharibu, miundombinu na hata kuwafanyia  Fujo Walimu
Hali   hii  imempelekea mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa geita,mwandisi Modest  Aporinali kufika shuleni    lengo   ni kuzungumza  na wanafunzi, uongozi, wa shule pamoja na walimu shuleni hapo.
Kutokana na suala hili walimu  wameanza kuelezea matatizo waliyonayo kama ambavyo  wanavyofafanua  hapa.

Aidha kutokana na maelezo hayo mkurugenzi  mtendaji wa halmashauri  ya  mji wa Geita,M odest Aporinali, amekutana  na wanafunzi na kutoa  maagizo  ambayo wanafunzi  wanatakiwa kuhakikisha wanayatekeleza.


Mkurugenzi aporinali, ameongeza kuwa hatakuwa na huruma kwa mwanafunzi ambae  ataonekana kwenda kinyume na kanuni na sheria  zilizowekwa shuleni hapo.

No comments:

Post a Comment