Tuesday 4 October 2016

PICHA:RAIS WA CONGO JOSEPH KABILA AHAIDI KUENDELEA KUITUMIA BANDARI YA DAR ES SALAAM



Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila akipokelewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli wakati alipowasili katika jengo la Mamlaka ya Bandari ya Tanzania kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi mapema hii leo jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila kushoto pamoja na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli wakitoa heshima kwa wimbo wa Taifa wakati wa sherehe za kuwekaji jiwe la msingi katika Jengo la Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) mapema hii leo jijini Dar es Salaam ambapo Rais wa Kabila alikuwa mgeni rasmi.



Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania Bw. Deusdedit Kakoko akitoa neno la utangulizi kwa Marais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila na wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli (hawapo pichani) wakati wa sherehe za kuwekaji jiwe la msingi katika Jengo la Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) mapema hii leo jijini Dar es Salaam ambapo Rais wa Kabila alikuwa mgeni rasmi.



Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akielezea historia fupi ya mradi “One Stop Centre” ulio chini ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kabla ya sherehe za uwekaji jiwe la msingi uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila mapema hii leo jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akisisitiza jambo kwa wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria sherehe za kuwekaji jiwe la msingi katika Jengo la Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) mapema hii leo jijini Dar es Salaam ambapo Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila alikuwa mgeni rasmi.



Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Wakandarasi wa Jengo la Mamlaka hiyo wakimskiliza kwa makini Mgeni Rasmi Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila wakati alipokuwa akielezea nia ya nchi yake kuitumia bandari ya Dar es Salaam mapema hii leo wakati wa uzinduzi wa jengo la kitega uchumi la mamlaka hiyo “One Stop Centre” mapema hii leo jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila akielezea dhamira ya nchi yake kuitumia bandari ya Dar es Salaam kwa wafanyakazi wa mamlaka hiyo (hawapo pichani) wakati wa sherehe za kuwekaji jiwe la msingi katika Jengo la Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) mapema hii leo jijini Dar es Salaam ambapo Rais wa Kabila alikuwa mgeni rasmi.



Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa jiwe la msingi katika jengo la kitega uchumi la Mamlaka ya Bandari Tanzania “One Stop Centre” mapema hii leo jijini Dar es Salaam ambapo Rais wa Kabila alikuwa mgeni rasmi.

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi pamoja na Mawaziri toka Kongo (DRC) na Tanzania. 

No comments:

Post a Comment