Wednesday 19 October 2016

MAGONJWA YASIOAMBUKIZWA TISHIO KWA VIFO VYA WATOTO NCHINI



 Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu

Imeelezwa kuwa asilimia 30 ya vifo vyote nchini vinavyotokea kwa watu wenye umri wa kuanzia miaka 15 na kuendelea, vinatokana na magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza kama vile kisukari, saratani, msukumo wa damu na magonjwa sugu ya mfumo wa hewa.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari wa Magonjwa yasiyo ambukiza Tanzania, Dkt. Andrew Swai amesema, ili kuepukana na magonjwa ya aina hiyo Serikali kupitia wataalam mbalimbali wa afya wanawajibu wa kuhakikisha wanatoa elimu ya kutosha kwa umma juu ya athari na namna ya kukabiliana na magonjwa hayo

Amesema magonjwa hayo yanasababishwa na mtindo wa maisha hasa kutokufanya mazoezi ya mwili pamoja na kutumia vitu vyenye sukari na chumvi nyingi.

Dkt. Swai amesema kati ya magonjwa hayo, ugonjwa wa 'presha' unaonekana kuongoza kwa vifo kwani ugonjwa huo husababisha vifo kwa asilimia 27 kutokana na kutokuwa na dalili na mara nyingine watu kuhisi kuwa wamerogwa.


Chama cha Madaktari wa Magonjwa yasiyo ambukiza Tanzania kimetoa wito kwa vyombo vya habari nchini kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wanaripoti na kuandika taarifa za magojnwa hayo kwani ndio yanaogoza kwa kusababisha vifo.

No comments:

Post a Comment