Friday 7 October 2016

PICHA:WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO PROF MAKAME MBARAWA ATEMBELEA KIVUKO CHA MAGOGONI/KIGAMBONI



Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa akipata maelezo ya ujenzi wa kivuko kipya cha Mv Kazi kutoka kwa Mkandarasi wa Kivuko hicho Mhandisi Major Songoro wa Kampuni ya Songoro Marine Boat Yard.

Kivuko Kipya kwa ajili ya Magogoni/Kigamboni kitakachoitwa MV. Kazi kikiwa katika hatua za awali za Ujenzi wake. Kivuko hiki kitakuwa na uwezo wa kubeba tani 170 sawa na abiria 800 pamoja na magari 22 kwa wakati mmoja.

Sehemu ya juu (deck) ya kivuko kipya cha Mv Kazi ikiendelea kujengwa. Kivuko hiki kitakuwa na uwezo wa kubeba tani 170 sawa na abiria 800 pamoja na magari 22 kwa wakati mmoja.
Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Kulia) akitoa Maelekezo kwa kuhusu upatikanaji kwa haraka kwa  Kivuko cha Mv Kazi ili kurahisiha huduma ya vivuko kwa JJijji la Dar es Salaam na vitongoji vyake wakati  alipotembelea kujjionea ujenzi wa kivuko hicho. Wa pili kutoka kushoto ni Mhandisi Jamal Waziri na kushoto ni Mtendaji Mkuu wa TEMESA Dr. Musa Mgwatu.

Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Profesa Makame Mbarawa akifafanua Jambo kwa Abiria wanaotumia vivuko vinavyotoa huduma kati ya Magogoni na Kigamboni alipotembelea Kivukoni hapo. Wa nne kulia waliosimama ni Mtendaji Mkuu wa TEMESA Dr. Musa Mgwatu.

Abiria wakishuka katika Kivuko cha MV. Magogoni upande wa Kigamboni, Kivuko cha Magogoni kilifanyiwa ukarabati mkubwa mwezi Mei 2016 na sasa kinaendelea kutoa huduma kwa wananchi wanaotumia kivuko hicho.

No comments:

Post a Comment