Friday 20 October 2017

WAMILIKI VIWANDA VYA KUCHAMBUA PAMBA WATOE MBEGU MANYOYA


Waziri wa Kilimo,Dr Charles Tizeba akizungumza na wadau wa kilimo cha pamba kwenye ukumbi wa mikutani wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Geita juu ya kuendelea kuboresha kilimo cha Pamba Mkoani Humo.
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Meja Jenerali Msataafu Ezekiel Kyunga akielezea namna ambavyo Mkoa umejipanga katika Kilimo cha zao la pamba kwenye msimu wa mwaka huu.
Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akiandika taarifa ambayo ilikuwa ikiwakilishwa na Mkuu wa Mkoa juu ya Kilimo cha Pamba.
Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba akisikiliza kwa makini maeleo ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.
Wajumbe wa Kikao hicho pamoja na wadau wa pamba Mkoani Geita.
Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba,akisisitiza wananchi kuendelea kulima pamba kutokana na serikali kuboresha baadhi ya changamoto ambazo zilikuwa ni kikwazo.  


Na.Joel Maduka 



Waziri wa Kilimo Dr Charles Tizeba amewataka wamiliki wa viwanda vya kuchambua pamba kupeleka mbegu za Pamba kwenye kiwanda cha kuzitolea manyoya cha Q-Ton na kwamba watakaokiuka hawatanunua Pamba msimu ujao.
Akizungumza na wadau wa pamba mkoani Geita, Dr Tizeba amesema atakayeshindwa kupeleka mbegu kwenye kiwanda cha kuzichakata, hatafanya biashara hiyo tena.
 “Najua kuna maginner wanne hapa sasa  atakayegoma kupeleka  pamba mbegu  Q-ton hanunui pamba mwaka kesho, wanapaswa kupeleka mbegu zitolewe manyoya ziende kwa wananchi ili wapate mbegu bora, katika hili sitabembelezana na mtu” alisisitiza Tizeba.
Alisemesema serikali ya kijiji ni vyema ikasimamiwa kikamilifu na halmashauri husika wakati wa ugawaji wa mbegu kutokana na kuendelea kwa malumbano yasiyo mazuri kwenye shughuli za kilimo cha pamba.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga amezitaka Halmashauri kuwajibika kuhakikisha zinabeba dhamana ya kilimo cha mkataba kwa Mkulima.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bukombe Nicas Mayala amesema wako tayari kutekeleza agizo hilo la waziri wa kilimo.

No comments:

Post a Comment