Monday 16 October 2017

JAMII YAASWA KUENDELEA KUWASAIDIA WATOTO WENYE UHITAJI NA WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU


Mwenyekiti wa  Jumuiya ya wanawake wa chama cha mapinduzi (CCM)Wilayani Geita Bi,Antonia Charles akikabidhi sababuni pamoja na vifaa vya shule kwa Mkurugenzi wa kituo cha kulelea watoto cha Bright light  na watoto ambao wanaishi kwenye Kituo hicho wakati wa kikao cha kwanza cha Jumuiya hiyo.

Katibu wa umoja wa wanawake wa chama cha mapiduzi  wilayani Geita,Bi Mazoea Salum ,Akizungumza na kusisitiza wananchi kujitolea kuwasaidia watoto waishio mazingira magumu.
Wajumbe wa kikao hicho wakifuatilia zoezi la utoaji wa msaada kwa watoto waishio mazingira magumu.
Uongozi wa Jumuiya ya wanawake wa chama cha mapinduzi wakiwa kwenye picha ya pamoja na watoto wa Bright light pamoja na Mkurugenzi wa Kituo hicho.
PICHA NA JOEL MADUKA.




Jamii Mkoani Geita imetakiwa kujitoa kwa moyo  wa kupenda kuendelea kuwasaidia watoto waishio katika mazingira magumu na wale ambao ni yatima.
Rai hiyo ilitolewa  na katibu wa umoja wa wanawake wa chama cha mapiduzi  wilayani Geita,Bi Mazoea Salum wakati  alipokuwa akiwakabidhi vifaa vya shule watoto wa kituo cha kulea watoto cha Bright light kwenye kikao cha kwanza cha jumuiya hiyo tangu uchaguzi kufanyika ndani ya chama.
Alisema  kuwa ni vyema jamii kwa ujumla kukumbuka kuwasaidia watoto ambao wana uhitaji  kwani hata kwenye vitabu vya Mungu vimeendelea kuelekeza kutoa msaada kwa yatima,wajane na wale ambao hawajiwezi  kwani  kufanya hivyo ni kumpendaza Mungu.
Aidha kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo hicho ,Methew Daniel ameelezea kuwa pamoja na kuendelea kufanya vizuri kwenye kituo hicho bado wanakabiliwa na matatizo ya jamiii kuendelea kukichukulia kituo hicho kuwa kina wafadhili jambo ambalo ni kinyume na kituo kilivyo.

No comments:

Post a Comment