Friday 13 October 2017

UKOSEFU WA WALIMU WA SAYANSI WAPELEKEA WANAFUNZI KUKIMBILIA MASOMO YA SANAA.

   
Translate message
Turn off for: Swahili
Wanafunzi wa kidato cha nne  Shule ya Sekondari Senga  wakiwa kwenye mahafari shuleni hapo.
Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi  ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafari hayo akiongozana na mwalimu Mkuu wa  shule ya Sekondari ya Senga wakati wa ukaguzi wa  ujenzi wa Mahabara shuleni hapo.
Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi akikagua ujenzi wa vyoo.

Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi pamoja na Mkuu wa shule ya Senga ,wakielekea kwenye madarasa ambayo yametengwa kwaajili ya wanafunzi kulala shuleni hapo.
Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi akikagua sehemu ya wanafunzi ambayo wanalala.
Eneo ambalo wanafunzi wamekuwa wakitumia kulala ambao ni wavulana.
Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi akiwa kwenye chumba ambacho kinatumika kama mahabara na hapa anaelezewa na mwanafunzi namna ambavyo mapigo ya moyo yanafanya kazi mwilini.

Mwalimu wa shule ya sekondari ya Senga  Mwl,Magoma Komesi Magero akiwatambulisha baadhi ya wageni waalikwa.
Walimu wa shule ya Sekondari ya Senga wakijitambulisha mbele ya Mgeni rasmi.
Wazazi wakiwa kwenye mahafari.

Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi akiwasisitiza wanafunzi kujisomea kwa bidii. Mkuu wa wilaya ya Geita akiwa kwenye picha ya pamoja na Walimu wa shule ya sekondari Senga.

PICHA NA JOEL MADUKA



Ukosefu  wa  walimu  wa  sayansi  imeelezwa  kuwa ni  kikwazo ambacho kimesababisha  wanafunzi  wengi  kutokuwa  na mwamko wa masomo hayo na kujikuta wengi wao wakikimbilia kwenye  masomo  ya  sanaa.
  
Hayo yamebainishwa na mwalimu wa shule ya sekondari ya Senga  Mwl,Magoma Komesi Magero kwenye mahafali  ya  nne,amesema  pamoja  na  shule  hiyo kuendelea  kufanya vizuri kwenye mitihani ya Kitaifa na mtihani wa utimilifu  bado inakabiliwa na changamoto  ya  walimu  wa masomo ya Baioloji  na  kemia.
Akisoma Risala kwa mgeni rasmi ambayo iliandaliwa na wanafunzi wa Kidato cha nne, Venasia Frances Amesema  shule hiyo inawalimu wa masomo ya sayansi watano tu ukilinganisha na idadi ya wanafunzi ambao wapo shuleni hapo huku akigusia na swala la vyumba vya madarasa.
Mgeni rasmi  kwenye mahafali ,Mkuu wa Wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi,ameitaka halmashauri kuongezea walimu wa masomo ya sayansi na pia amewapongeza walimu hao watano wa masomo ya sayansia pamoja na uchache wao wamejitahidi kufanya vizuri kwenye masomo hayo.
Jumla  ya wanafunzi  ambao  wamesajiliwa  kufanya mtihani kwenye shule ya sekondari ya  Senga  ni  97.

No comments:

Post a Comment