Monday 7 August 2017

MCHUNGAJI AMTABIRIA USHINDI RAILA ODINGA




Mchungaji wa Kanisa la EAGT Majengo mapya tawi la Nyankumbu wilayani na Mkoa wa Geita David Joseph Magige ,akizungumza na waumini wa Kanisa ambalo analiongoza Juu ya utabiri na maono kuhusu uchaguzi wa Nchini Kenye kwenye ibada ya jana.
Ikiwa kesho wananchi nchini Kenya wanatarajia kupiga kura ya kumchagua Rais wa Nchi Hiyo ,Mchungaji wa Kanisa la EAGT Majengo mapya tawi la Nyankumbu wilayani na Mkoani Geita David Joseph Magige  amemtabiria ushindi mgombea wa Muungano wa vyama vya siasa NASA ,Raila Odinga Kuwa rais wa Kenya.

Mchungaji Magige,katika mahubiri yake kwenye ibada ya Jana Kanisani Hapo amesema utabiri wake unatokana na maono aliyofunguliwa na Mungu katika sala na maombi yake.

“Ni mara ya tatu sasa Rohoo mtakatifu amekuwa akinifunulia maono ingawa nimekuwa ni muoga sana kujitokeza na kutamka mbele za watu mara ya kwanza ni uchanguzi Mkuu wa nchini kwetu nilioteshwa kuwa Rais ambaye atashinda ni Magufuli lakini sikuweza kusema,na bado hata Marekani pia wakati wa mchakato wa uchaguzi nilipata maono kuwa ambaye atakalia kiti cha urais ni Donald Trump lakini pia nilisita kusema nilimwambia Mke wangu awamu hii nasema ni Raila Odinga ndiye ambaye atashinda kiti cha Uraisi maana ni changuo la Mungu”Alisema Mchungaji Magige.

Aidha, mchungaji Magige amewataka waumini wake pamoja na Watanzania kwa ujumla  kuendelea kuliombea taifa la Kenya ambalo litafanya uchaguzi mkuu August 8 mwaka huu na pia kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli.

Uchaguzi huo unawahusisha wagombea urais wawili ambapo Rais anayemaliza muda wake Uhuru Kenyata na Mgombea anayeungwa mkono na umoja wa vyama vya upinzani NASA Bw. Raila Odinga.

No comments:

Post a Comment