Tuesday 13 December 2016

SERIKALI YA CHINA KUJENGA KIWANJA CHA KISASA CHALINZE



Serikali ya China imetoa ufadhili wa ujenzi wa uwanja wa Michezo kwa shule ya msingi Msoga iliyopo halmashauri ya wilaya ya Chalinze.
Akizungumza katika hafla ya kuoneshwa eneo patakapojengwa uwanja huo  Rais mstaafu wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete  ameishukuru serikali ya China kwa msaada huo kwakuwa Michezo ni Kitu muhimu kwa watoto huku akitoa rai kwa halmashauri ya chalinze kulinda eneo hilo.

Kwaupande wake mwakilishi wa balozi wa China amesema kuwa China inajivunia uhusiano mwema uliopo kati ya China na Tanzania,na watahakikisha wanajenga uwanja huo kwa wakati ili kuwapa fursa watoto kufurahia michezo.

Nae Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete ametoa rai kwa wananchi wake kuhakikisha eneo lililotengwa linalindwa ili dhamira ya china kujenga uwanja huo itimie


Ufadhili wa ujenzi wa uwanja huo wa michezo kwa watoto wa Msoga ni muendelezo wa ufadhili wa China katika kijiji cha Msoga baada ya kujenga shule ya msingi Msoga.



No comments:

Post a Comment