Thursday 29 December 2016

MKUU WA MKOA WA GEITA AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI WA VITAMBULISHO MKOANI HUMO




Mkuu wa Mkoa wa Geita ,Meja jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga akikabidhi vitambulisho vya watumishi kwa mwakilishi kutoka wilaya ya Mbongwe Bw,Paul Cheyo wakati wa zoezi la uzinduzi wa vitambulisho vya Taifa Mkoani Geita.




Mkuu wa Mkoa wa Geita ,Meja jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga,akionesha kitambulisho chake baada ya kukabidhiwa.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja jenerali mstaafu Ezekiel Kyunga amewataka watendaji kusimamia kwa umakini zoezi la vitambulisho vya Taifa litakapoanza ili kuakikisha kila mwananchi anapata kitambulisho hicho lengo ni kujua na kuwatambua wananchi ambao wapo Mkoani humo.

Hayo ameyasema wakati wa uzinduzi wa zoezi la ugawaji wa  vitambulisho vya Taifa(NIDA) lililokuwa linaambatana na utoaji wa vitambulisho kwa watumishi wa serikali.

Kyunga amewataka wananchi kuwa na ushirikiano kufanikisha zoezi hilo ambalo linatarajia kuanza mwezi January mwakani  baada ya kuwa limemalizika kwa watumishi wa serikali Mkoani Humo.

Ameeleza kuwa shughuli ya uandikishaji wa vitambulisho hivyo utasaidia   kujua ni idadi ya wananchi wangapi ambao wapo kwenye Mkoa wa Geita lakini pia katika kata,mitaa na vitongoji.


Pia amewaasa wale ambao sio watanzania  lakini wapo Mkoani kwa shughuli mbali mbali zikiwemo za uwekezaji  kuacha kujiingiza kwenye usajili huo na badala yake  wasubilie taratibu ambazo zitatangazwa na tume ya Taifa vitambulisho vya uraia.

No comments:

Post a Comment