Monday 12 December 2016

SALAAM ZA LOWASSA KATIKA SIKUKUU YA MAULID



Nachukua nafasi hii kuwatakia kheri na baraka waislam wote nchini katika kuadhimisha siku hii ya kuzaliwa kwa kiongozi wao Mtume Muhammad SAW.

Waislam kama walivyo watanzania wa dini nyingine wamekuwa nguzo muhimu katika kujenga amani, upendo na utulivu nchini kwetu, na hii yote ni kutokana na mafundisho ya kiongozi wao huyo.

Ni rai yangu kwa watanzania wote wakiwemo watawala kuwa tunapo sherehekea siku hii tutimize kwa vitendo mafundisho ya bwana Mtume ambaye ni mmoja wa mitume wa mwenyezi mungu kwa kuheshimiana, kuvumiliana na kupendana.

Edward Lowassa

Waziri mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu - Chadema.

No comments:

Post a Comment