Friday 16 March 2018

UHABA WA VYOO WAWATESA WAFANYABIASHARA KATIKA SOKO LA CCM, KATORO




Baadhi ya wafanyabiashara katika soko la chama cha mapinduzi Ccm lililopo kata ya katoro Mkoani Geita wamekiomba chama hicho kuwajengea choo bora kwakuwa kilichopo kwasasa hakikidhi mahitaji ukilinganisha na idadi ya watu wanao ingia na kutoka ndani ya soko hilo.

Wakizungumza na storm habari baadhi ya wafanya biashara hao  Samweli  Jaksoni, Milanga Shukuru na Paulina Petro katika soko hilo wamesema wanapata wakati mgumu pindi wanapo hitaji huduma hiyo kwani choo kilichopo kwasasa nikidogo ukilinganisha na idadi ya watu kwenye soko hilo.

Sanjari na hayo wamesema chama cha mapinduzi kinatakiwa kuchukua hatua za makusudi kuwajengea choo bora katika eneo hilo kwani wanalipa pango la aridhi pamoja na ushuru kila siku huku wengine wakilipa mwisho wa mwezi.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara katika soko hilo Bw Charles Mlale amesema choo kilichopo kwa sasa siyo bora na kina idadi ya matundu manne hali inayo walazimu kwenda katika kaya jirani kuomba huduma ya kujisaidia.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ukusanyaji wa fedha wa chama cha mapinduzi Ccm kwenye soko hilo Bw Majaliwa Bukeke amekili kuwepo kwa changamoto hiyo nakusema kuwa wapo mbioni kutafuta mzabuni watakae ingia nae mkataba ikiwemo kujenga choo cha kisasa katika soko hilo.

No comments:

Post a Comment